![]()  | 
| Marehemu Hamida Urembo | 
Hamida na mumewe yahaya walibahatika kupata mtoto wa 
kike mwenye miaka mitatu sasa.Kwa mujibu wa dada wa Hamida ndoa yao 
ilikuwa ya misuko suko sana.Mume alikuwa sio mwaminifu mara nyingi 
alikuwa akizini nje.Ukiacha hilo alikuwa akimpiga sana mkewe mpaka 
kumzimisha.
Matatizo ambayo ndugu walikuwa wakiyajua na 
walishasuluhisha mara nyingi na Hamida kurudi kwa mume kuendelea na 
maisha.Hii ya mwisho ndio ilikuwa kubwa zaidi.Mume alikuwa akimtongoza 
housegirl hapo nyumbani na alipokuwa kesho housegirl akamfahamisha mama.
Akamueleza jinsi gani muwewe amekuwa akimsumbua 
kumtaka kimapenzi.Hamida akamwambia
anataka tu uthibitisho kama ni kweli.Siku ya siku Yahaya akamlazimisha 
Hamida kwenda kwao na Hamida akakubali akijua kuna jambo.Akasindikizana 
na mumewe mpaka kituoni mume akijua mkewe hayupo kumbe mke aligeuzia 
njiani akarudi nyumbani akajificha chini ya uvungu chumbani kwa 
housegirl wake.Baadae mume akawasilia na housegirl kuwa anarudi 
nyumbani,aliporudi akaendelea kuomba mambo tena akavua nguo kabisa 
akabaki na boxer.Wakati huo yupo chumbani kwao na mkewe.Housegirl 
akamwambia wahamie chumbani kwako hapo sio salama.Basi wakahamia 
chumbani na akawa ndio anamuinamisha dada ili amfanye Hamida akatoka 
chini ya uvungu ili kumuokoa dada na kumuonyesha mumewe kuwa alikuwepo 
na amejua usaliti wake.Na alipokuwa chini ya uvungu alikuwa akirekodi 
kila kitu kwenye simu na alipotoka na picha akapiga.
![]()  | 
| Huyu ndiye Yahaya aliyekuwa mume wa marehemu Hamida | 
Hamida alitoka
hapo akashitaki kwao na kwao wakamwambia aende kwa mjomba wa mumewe 
kumueleza matatizo ya mtoto wao. Alipofika kwa mjomba akaambiwa wanaume 
ndivyo walivyo avumilie tu arudi kwa mumewe.
Hamida
akarudii kwao akiwa hana hana raha lakini uamuzi aliouchukua ni kuachana
 na mumewe kwani alikuwa kashachoka. Wakawa wakivutana sana mume
akimsihi arudi nyumbani walikokuwa wakiishi Mbagala ila Hamida 
hakuridhia.
Hamida alishaenda mpaka Bakwata ili mumewe aamriwe kutoa talaka.
Mwisho wa Hamida kuonekana nyumbani ni siku ambayo 
yeye na ndugu zake walikuwa waende kijijini kwao kwenye viwanja 
walivyopewa na babu yao.Ila siku hiyo Hamida alitoa udhuru kuwa haendi 
na akamtaarifu mama yake kuwa Yahaya kamuita akachukue vitu vyake 
vilivyobakia.Mama akamkatalia kwenda
akamwambia kuna kaka zake wakubwa aache wataenda kuvifata kwani huyo 
mume ni mshenzi anaweza kumfanyia kitu kibaya.Hamida akamwambia mama 
anataka kwenda mwenyewe kwani kuna vyeti vyake muhimu akavichukue.
Basi mama akamuacha aende kishingo upande lakini mama 
akamwambia basi nenda hata na mdogo wako.Akaenda na mdogo wake lakini 
kufika kule mume akamkatalia mdogo mtu kuingia ndani.
Wakabishana sana kwa nini asiingie mdogo mtu kuepusha shari akaenda kukaa kwa jirani
asubiri kuitwa. Akakaa na muda kupita kukawa kimya akajua wale wameelewana ndio maana hakuna makelele hivyo akaendelea kusubiri.
Akakaa weee mpaka jioni giza lilipoanza kuingia kidogo
 Yahaya akampigia simu kwa kutumia simu ya Hamida akimwambia aondoke tu 
arudi nyumbani wao wameshaondoka na vyombo wamebeba.
Mdogo mtu akaondoka kurudi nyumbani kwao Tabata akijua mke na mume wameelewana kumbe dada yake ameshakufa ndani.
Mdogo mtu akafika nyumbani saa mbili usiku na 
kumwambia mama jinsi Hamida alivyomuudhi kamuacha yeye kwa jirani na 
akaondoka na mumewe Yahaya.Mama
machale yakamcheza akanyanyua simu akampigia Yahaya kumuuliza mwane yupo
 wapi.Yahaya akamjibu kuwa ameachana nae kitambo mama akamwambia sio
kweli mwanangu hawezi kuchelewa kurudi nyumbani na hana kawaida 
hiyo.Yahaya akamjibu atarudi tu Hamida mtu mzima.
Mamam tayari alishajua kuna jambo akampigia simu baba 
Hamida aliyekuwa Arusha kumtaarifu kilichotokea. Baba Hamida akampigia 
Yahaya lakini hakupokea simu.Wasiwasi ukazidi kutanda na ndugu kupeana 
taarifa zaidi.Asubuhi kulipokucha wakaenda Mbagala kwa Yahaya lakini 
wakatoa taarifa polisi.Polisi wakawaondoa wasiwasi kwamba hao wanajuana 
wenyewe labda wameamua kukumbushiana.
Ndugu hawakuridhika wakaenda kwa mjumbe awaruhusu 
wavunje nyumba waingie ndani
pengine kamfungia ndani maana ilikuwa kawaida yake kufanya hivyo 
kumfungia Hamida ndani.Basi mjumbe akaruhusu mlango uvunjwe walipoingia 
ndani palikuwa patupu hawakuona kitu wala dalili za mauaji.Kuna chumba 
ambacho ni stoo hicho walishindwa kufungua na mjumbe akawaambia hiyo ni 
stoo wanawekaga mavitu yamejazana humo basi wakakiacha wakaondoka.
Hawakuishia hapo bado waliendelea kumsaka Hamida bila mafanikio.
Hamida alipotea toka jumapili iliyopita,jumanne juzi 
kila mtu wakapanga kila mtu akamtafute popote pale anapoona anaweza 
kumpata.Mama akaenda kwenye maombi kanisani wakati muislam,dada akaenda 
blue pearl kazini kwa Yahaya
na huku majirani Mbagala wakaanza kuona inzi na harufu kali ikitoka 
nyumbani kwa Yahaya.Ikabidi mjumbe apige simu kwa mama Hamida kumueleza 
kinachoendelea polisi wakaitwa,nyumba ikavunjwa ili kutafuta harufu 
inatokea wapi.Wakavunja kile chumba cha stoo na kukuta mwili wa Hamida 
umeshaanza kuharibika.Kanyongwa na kamba ya katani na kitenge kafungwa 
puani na mdomoni.Mwili wake ukawekwa kwenye mfuko akajaziwa mito na 
manguo nguo na tendegu la kitanda kawekewa shingoni.
Ndugu, polisi wakachukuwa mwili kwa ajili ya msiba na mazishi wakati huo Yahaya alishakimbia siku nyingi hajulikani alipo.
Hamida alizikwa jana kule kwa babu yake Mzenga 
uzaramuni walipokuwa waende  kwenye mashamba waliyopewa. Msiba upo 
nyumbani kwao Tabata. Mrehemu ameacha mtoto wa kike wa miaka mitatu 
anaitwa Tayana.
Habari hii inaendelea tena kesho katika heka heka za leo ndani ya leo tena ya clouds fm.
R.I.P Hamida na tunatoa pole kwa familia nzima ya Urembo kwa msiba





poleni wafiwa, hasa mtoto! roho yauma haswa
ReplyDelete