Watuhumiwa
 wawili wa kesi ya mauaji dhidi ya aliyekuwa Mwenyekiti wa Halmashauri 
ya Wilaya ya Rungwe, John Mwankenja, Kelvin Myovela(kushoto), 
aliyehukumiwa kifungo cha miaka saba jela na David Mwasipasa(Kulia) 
amehukumiwa kunyongwa hadi kufa baada ya kupatikana na hatia katika 
Mahakama kuu kanda ya Mbeya.
Mhukumiwa
 namba moja wa kesi ya mauaji dhidi ya aliyekuwa Mwenyekiti wa 
Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe, Hakimu Mwakalinga(kushoto) amehukumiwa 
kunyongwa hadi kufa na mwenyeshati la Bluu ni Obote Mwanyingili 
amehukumiwa miaka saba jela kwa kumhifadhi mtuhumiwa.(Picha na Ezekiel 
Kamanga, Mbeya)
Awali
 kabla ya kusoma kwa hukumu hiyo Mwendesha mashtaka wa Serikali., 
Archiles Mulisa, aliwataja watuhumiwa wote wanne kuwa ni Hakimu
 Mwakalinga, Daudi Mwasipasa, Obote Mwanyingili na Kelvin Myovela 
wanaokabiliwa na tuhuma za kumuua kwa maksudi aliyekuwa Mwenyekiti wa 
Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe John Mwankenja.
 
Alisema
 watuhumiwa hao wenye kesi namba 131/2012 walitenda kosa hilo Mei 19, 
2011 katika kijiji cha Mpandapanda, Kata ya Kiwira Wilaya ya Rungwe 
Mkoani Mbeya.
  
Mulisa
 aliyekuwa akisaidiwa na Wakili wa Serikali Lugano Mwakilasa kwa upande 
wa mashtaka huku  Watuhumiwa wakitetewa na Mawakili wawili ambao ni 
Victor Mkumbe na Simon Mwakolo. 
 
Mulisa
 alidai mahakamani hapo kuwa kesi inayowakabili  watuhumiwa hao 
walilitenda Mei 19,2011 kwa kumuua kwa maksudi John Mwankenja kinyume na
 kifungu cha 196 sura ya 16 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.
 
Akisoma
 hukumu hiyo Jaji Karua ambaye alianza majira ya saa 14:37 mchana na 
kukamilisha saa 15:37 alisema katika kesi hiyo upande wa mashtaka na 
utetezi haubishaniwi kuhusu kifo cha marehemu.
 
Aliongeza
 kuwa pande hizo mbili pia hazibishaniwi kuhusu ripoti za kitaalamu na 
dhamira za mauaji hayo bali kinachobishaniwa ni uhusika wa watuhumiwa 
hao dhidi ya mauaji hayo.
 
Alisema
 katika kutetea hoja zao upande wa mashtaka ulileta mashahidi 11 ambao 
wote kwa pamoja  wakiongozwa na shahidi namba moja waliwatuhumu 
washtakiwa kuhusika na tukio hilo.
 
Shahidi
 huyo namba moja Weston Jacob(17) mkazi wa Kiwira Mwanafunzi kidato cha 
Tatu katika shule ya Sekondari Kipoke ambaye pia ni Mjomba wa marehemu 
ambaye aliiambia mahakama kuwa siku ya tukio akiwa nyumbani akijisomea 
majira ya 2: 30 usiku ambapo marehemu alifika nyumbani na kupiga honi ya
 gari akitaka afunguliwe mlango.
Mbali
 na ushahidi huo Jaji Karua alisema pamoja na ushauri wa wazee wa baraza
 la mahakama ambao pia wanawatuhumu washtakiwa hao kuhusika na tukio 
hilo nae anakubaliana nao lakini siyo kwa watuhumiwa wote.
 
Kutokana
 na ushahidi huo alisema Mshtakiwa namba moja na namba mbili ambao ni 
Hakimu Mwakalinga na Daudi Mwasipasa wanatiwa hatiani kuhusika moja kwa 
moja na mauaji kutokana na ukiri wao kwa mlinzi wa amani, Mchukua 
maelezo na  vipimo vya vinasaba.
 
Alisema
 Mshtakiwa namba tatu Obote Mwanyingili yeye anatiwa hatiani kutokana na
 kosa la kumhifadhi mtuhumiwa namba moja baada ya kutoka kufanya mauaji 
hivyo yeye hausiki moja kwa moja na kosa hilo.
  
Jaji
 karua alisema kwa upande wa mshtakiwa namba nne Kelvin Myovela anatiwa 
hatiani kutokana na kuhifadhi silaha iliyotumika nkatika mauaji hayo 
ingawa hakusika na kitendo hicho moja kwa moja.
 
Aliongeza
 kuwa kutokana na kifungu cha sheria cha mwenendo wa makosa ya jinai 
kifungu namba 300 na 217 washtakiwa namba tatu na namba nne wanatiwa 
hatiani na mahakama.
 
Mwendesha
 mashtaka wa Serikali Archiles Mulisa, aliiambia mahakama hiyo kwamba 
itoe adhabu kali kutokana na kitendo alichofanyiwa marehemu na iwe 
fundisho kwa watu wengine.
 
Kwa
 upande wa utetezi ambao siku ya hukumu uliwakilishwa na Wakili Merick 
Luvinga alisema mahakama iwanee huruma washtakiwa kwa kuwa wote umri wao
 ni mdogo wanaweza kujifunza na kurudi kuungana na jamii pia ni kosa lao
 la kwanza hivyo wasipewe adhabu kali.
 
Kutokana
 na utetezi huo, Jaji Karua alisema kutokana na ushahidi uliotolewa 
mahakamani hapo kuthibitisha kuhusika pasipo shaka kwa washtakiwa namba 
moja na namba mbili hivyo adhabu yao ni kunyongwa hadi kufa.
 
Aliongeza
 kuwa Mshtakiwa namba tatu Obote Mwanyingili anayehusika kumhifadhi 
mtuhumiwa wa kwanza ataenda jela miaka saba kwa kosa hilo sambamba na 
mshtakiwa namba nne  Kelvin Myovela aliyehifadhi silaha iliyotumika 
kwenye mauaji.
 
Alisema
 kutokana kosa hilo mtuhumiwa huyo atatumikia kifungo jela miaka saba 
ingawa pia tayari alikuwa amehukumiwa kifungo jela cha miaka 20 kwa kosa
 la kukutwa na silaha kinyume cha sheria.



0 comments:
Post a Comment
TOA MAONI YAKO HAPA....