SHILOLE na BARNABA warudiana tena!!




KUNA tetesi kuwa, penzi lililokuwa limekufa kati ya mwigizaji wa Bongo, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ na Mbongo Fleva, Elias Barnaba limerejea kwa ari, nguvu na kasi mpya.


“Hivi karibuni wawili hao walionekana chobingo, Mbeya kwenye Tamasha la Serengeti Fiesta na hata Dar pale Leaders Club, walikuwa "close" nyuma ya jukwaa katika gari la Shilole,” alisema mpashaji wetu.


Mwanahabari wetu aliwatafuta hewani wote, lakini Shilole ndiye aliyepatikana, akafunguka:

“Kwani tatizo lipo wapi tukirudiana? Mbona hamuwashangai akina Chris Brown na Rihanna? Mapenzi ni upofu acheni hizo,” alisema Shilole. 

Tupe maoni yako hapo chini..!

Share this article :

'LIKE' UKURASA WETU WA FACEBOOK HAPO CHINI...!

0 comments:

Post a Comment

TOA MAONI YAKO HAPA....

 

Copyright © 2010 GUMZO LA JIJI.

Like Us On Facebook
Follow Us on Twitter