CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimepata pigo baada ya Naibu
 Meya wa Manispaa ya Moshi, mkoani Kilimanjaro, Vicent Remoy, kufariki 
ghafla jana.
Akithibitisha kutokea kwa kifo hicho, Meya wa Manispaa 
hiyo, Jafary Michael (CHADEMA), alisema Remoy ambaye pia alikuwa ni 
Diwani wa Kata ya Kiboriloni, zahanati ya Jafary iliyoko katikati ya mji
 wa Moshi.
  
 
“Ni kweli amefariki, na mimi nimepokea taarifa hiyo dakika
 30 zilizopita, na kwa mujibu wa taarifa za awali, ni kwamba alienda 
kutizama afya yake hapo zahanati baada ya kuhisi kifua kuwa kizito 
wakati akiwa shambani kwake Msalanga,” alisema Michael.
Alisema mara 
ya mwisho kuzungumza naye kuhusu ugonjwa ilikuwa ni wakati wamesafiri 
kwenda nchini Ujerumani kwa ajili ya mazungumzo na serikali ya nchi hiyo
 ambako alimwambia kuwa amekuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa miguu 
(gauti).
Mstahiki Meya Michael ambaye pia ni mwenyekiti wa CHADEMA 
Manispaa ya Moshi, alisema chama kimepokea kifo hicho kwa mshituko 
mkubwa kutokana na ukweli kwamba Remoy ndiye alikuwa muasisi wa chama 
katika Manispaa ya Moshi.
  
“CHADEMA manispaa tumepokea kwa mshituko 
mkubwa kifo cha huyu mzee. Mbali ya kuwa muasisi wa chama, pia alikuwa 
kiungo muhimu kama mtu mzima kwa wanasiasa ambao ni vijana bila ya 
kujali itikadi za kisiasa,” alisema Michael.
Alisema pia marehemu 
alikuwa Diwani wa Kata ya Kiboriloni kwa vipindi vitatu mfululizo 
kuanzia mwaka 2000 hadi sasa, huku akiwa mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya
 CHADEMA katika Manispaa ya Moshi.
  
“Naweza
 sema alikuwa ni kiongozi mwandamizi ndani ya CHADEMA, na pia 
ameshikilia nafasi ya naibu meya kwa vipindi vyote vitatu. Mara ya 
mwisho alichaguliwa kwa kura zote ambazo zilipigwa na madiwani wa 
CHADEMA na CCM,” alisema Michael.
Alisema mwili wa marehemu 
umehifadhiwa katika hospitali ya rufaa ya KCMC na kwamba hadi sasa 
chanzo cha kifo chake hakijafahamika



0 comments:
Post a Comment
TOA MAONI YAKO HAPA....