WEMA AMUOGESHA MREMBO KWA POMBE

KATIKA kuonesha jeuri ya fedha, Wema Isaac Sepetu amefanya kufuru kama kawaida yake baada ya kumlowanisha mwili mzima kwa pombe za bei mbaya mrembo aitwaye Rehema Kimbu.
Mrembo Wema Sepetu akimwogesha Rehema Kimbu kwa pombe.
Tukio hilo lililoshuhudiwa na mwanahabari wetu lilijiri nyumbani kwa mwigizaji Aunt Ezekiel, Mwananyamala, Dar, Ijumaa iliyopita ambapo Wema na Aunt walimfanyia ‘sapraizi’ ya ‘bethidei’ Rehema ambaye ilikuwa siku yake ya kuzaliwa.
Rehema Kimbu akizidi kumwagiwa kilevi wakati wa sherehe yake ya kuzaliwa.
Katika hali ya kushangaza, Rehema ambaye ni shosti mkubwa wa Aunt alishtukia anamwagiwa pombe mfululizo aina ya Gordon’s na Jack Daniels huku mwigizaji Nice Chande akimmiminia chupa kubwa kadhaa za maji.
Rehema Kimbu akiwa kalowa mwili mzima baada ya kumwagiwa pombe na Wema (kushoto).
Muda mwingi Wema alikuwa akimmwagia Rehema pombe bila kushusha mkono.
Kufuatia kitendo hicho kilichoambatana na kelele nyingi za mastaa hao,  kilisababisha wapita njia kujazana getini kwa Aunt bila kujua kilichokuwa kikiendelea na kudhani Rehema alikuwa akipokea kipigo.

Vicheko: Rehema akiangua kicheko baada ya sherehe yake kunoga.

Tupe maoni yako hapo chini..!

Share this article :

'LIKE' UKURASA WETU WA FACEBOOK HAPO CHINI...!

0 comments:

Post a Comment

TOA MAONI YAKO HAPA....

 

Copyright © 2010 GUMZO LA JIJI.

Like Us On Facebook
Follow Us on Twitter