VIDEO: AFUNGWA MIAKA 10 BAADA YA KUKAMATWA AKIMBAKA MBUZI....!!

Jamaa mmoja mwenye umri wa miaka 28 amehukumiwa kwenda jela miaka kumi mara baada ya kukutwa na hatia ya kufanya tendo la ngono na mbuzi.
Katana Kitsao





Katana Kitsao Gona toka Malindi nchini Kenya wiki iliyopita alikiri kufanya ngono na mnyama. 

Shuka chini kuangalia Video hiyo..... 
Mbuzi huyo wa kike kwa utulivu alikuwa pembeni ya chumba cha mahakama wakati hukumu hiyo ilipokuwa inatolewa. Jamaa huyo alikamwatwa mnamo tarehe 25 Novemba mara baada ya mkazi mmoja wa eneo hilo kumbamba akiwa uchi wa mnyama akimla uroda mbuzi huyo ambaye alikuwa amefungwa kamba, hii ni kwa mujibu wa The Star.
Mbuzi

Mmiliki wa mbuzi huyo alifahamishwa na kufika eneo la tukio akiwa na majirani wengine ambao pia walimshuhudia Gona akiwa anafanya ngono na mnyama.

Jamaa alikamatwa na polisi na vipimo vya hospitali vinakaonyesha kweli kwamba tukio la ngono lilifanyika.

Gona aliomba msamaha kwa mahakama kwa kujitetea kuwa mke wake ni mlemavu na anamtegemea yeye ila mahakama ikajibu kuwa kosa hilo ni kubwa na akapewa siku 14 za kukata rufaa.
VIDEO:

PICHA ZINATISHA: MZEE MMOJA AGONGWA NA GARI NA KUSAGIKA MGUU ALIPOKUWA ANAVUKA BARABARA,KILIMANJARO....

.
MZEE huyu wa jamii ya kabila la wamasai aliyetambulika kwa jina la ''Tulito'' Mkazi wa KIA njia panda ya kuelekea uwanja wa ndege wa Kilimanjaro International Airpot, amepata ajali mbaya ya kugongwa na fuso alipofanya jaribio la kuvuka barabara hiyo ya lami ambayo magari huenda mwendo kasi.
 
Kwa mujibu wa chanzo cha habari kutoka mkoni kilimanjaro 
kimedai kwamba gari hilo aina ya FUSO halikusimama baada ya kumgonja mzee Tulito, lilitokomea..! Raia waliokuwa karibu na eneo la tukio hawakufanikiwa kunasa hata namba za gari hilo, Mzee tulito aliwahishwa Hospitali wilayani boma kwa matibabu zaidi.

CHANZO : MATUKIO NA MICHAPO

PICHA:TIMBWILI LAZUKA BAADA YA MWANAUME MMOJA KUGONGANISHA MKE NA KIMADA CHAKE WALIOKUJA KUMPOKEA AIRPORT....

 .
MWANAUME mmoja aliyeelezwa kuwa ni tajiri mwenye nazo mjini, amezua tafrani na kusababisha timbwili la nguvu kwa dakika kadhaa baada ya kugonganisha wanawake wawili waliodaiwa kuwa chini ya miliki yake kwa wakati mmoja, subiri hapohapo tukujuze!
 
Mtiti huo uliovuta hisia za wengi ulichukua nafasi Ijumaa iliyopita, mishale ya saa sita na dakika zake usiku, pande za Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere ‘JNIA’ ambapo mwanaume huyo ambaye jina lake halikupatikana mara moja alitua na Ndege ya Shirika la Kenya.
ANGALIA SINEMA
Hali ya hewa ilikuwa ya kuridhisha kabisa katika eneo la uwanja wa ndege wakati paparazi wetu akiwa kwenye sehemu maalum ya kusubiria abiria wanaotua uwanjani hapo wakitokea nje ya nchi.
Paparazi wetu alikuwa akimsubiri mgeni wake lakini kama ilivyo kawaida ya wanakikosi cha Oparesheni Fichua Maovu ‘OFM’ alikuwa na zana zake za kazi kama kawaida.


Wakati wageni wakianza kutoka, ghafla zilisikika kelele pembeni mwa sehemu aliyokuwa paparazi wetu, akajiuliza kunani? Akaweka zana zake za kazi sawa kisha akajongea eneo la tukio.
VARANGATI LA NGUVU
Kamera za Risasi Mchanganyiko zilishuhudia wanawake wawili wakikunjana na kupigana makonde huku mmoja akimshutumu mwenzake kumwibia mumewe (haikujulikana kama ni wa ndoa). Alisema: “Wewe mpumbavu mwizi wa waume za watu, nitakukomesha leo. Si umezoea kuiba waume za watu? Sasa utanijua mimi ni nani?”


Mwanamke huyo aliyeonekana kuwa na jazba, alikuwa na watoto wake wawili waliovalia sare za shule ambao walikuwa wakimvuta na kumsihi aachane na ugomvi.
MSHANGAO NI HUU!
Sekeseke wakati likiendelea, yule mwanamke ambaye alikuwa akidai kuibiwa mumewe kwa muda mrefu na mwanamke huyo, watoto wake wawili walikuwa naye sambamba huku wakijaribu kumtuliza ingawa kiumri ni wadogo.
Mwanamke aliyedaiwa kuchukua mume wa mwenzake naye alikuwa na mtoto wake mmoja ambaye alikuwa akimvuta akitaka kumtoa mikononi mwa mwanamke aliyedaiwa kuwa mmiliki rasmi wa tajiri huyo.


Mshangao mkubwa ni kitendo cha watoto hao wote kuwa wamevaa sare za shule, tena zikionekana kuwa za shule moja – maswali yalikuwa mengi kuliko majibu!
“Hawa watoto sijui wamekuja na huyu jamaa? Maana wanaonekana kama wanasoma shule moja na wapo na vifaa vyao vyote vya shule. Hapa hata haileweki jamani,” alisikika dereva teksi mmoja aliyekuwepo eneo la tukio.


MAELEZO MENGINE
Mashuhuda walisema, awali tajiri yule wakati anatoka katika sehemu maalum ya abiria wanaoingia nchini, alikimbiliwa na mwanamke yule anayedaiwa kuwa kimada na kumpokea kisha kumbusu na kumpa pole kwa safari.

“Tatizo lilianzia pale yule mwanamke mwembamba mwenye nguo nyekundu alipoenda kumpokea jamaa. Alimfuata na kumkumbatia kisha akambusu, basi hapo tafrani ikatokea. Yule mke wa jamaa alikwenda haraka na kumvamia kisha kuanza kumpiga,” alisikika mmoja wa mashuhuda hao.
TAJIRI AWAZODOA WALIOMSHANGAA!
Wakati tafrani ile ikiendelea, mwanaume huyo aliwaingilia kati na kuwaamulia, jambo lililozidisha watazamaji wa sinema hiyo ya bure kushangaa.

Katika hali ya kushangaza, tajiri huyo aliwananga watu waliokuwa wakimshangaa akisema: “Sasa kipi cha ajabu? Ni mwanaume gani hapa ambaye hajawahi kufumaniwa? Haya ni mambo ya kawaida, endeleeni na shughuli zenu nitamaliza hii ishu mwenyewe.”

Juhudi za tajiri huyo kuwaachanisha zilizaa matunda, kwani zaidi ya kutumia nguvu, alionesha ‘uanaume’ wake kwa wanawake hao ambao walikubali kuachana na ugomvi huo ingawa kila mmoja alionekana kuwa na hasira na mwenzake.
Baadaye yule mwanamke aliyedaiwa kuwa ndiye mke halali wa tajiri yule, aliondoka naye wakiwa na watoto wao wawili, mwingine akaondoka na mtoto wake.

GPL

SINEMA YA BABY MADAHA NA DIAMOND BADO INAENDELEA,DIAMOND NAE AFUNGUKA NA KUMPONDA BABY MADAHA....

.
Baby Madaha akiwa na Diamond.
ACHANA na mabifu yaliyotangulia, hili ni jipya kabisaa! Msanii wa sinema na Bongo Fleva, Baby Joseph Madaha ameingia kwenye bifu zito na Nasibu Abdul Jumaa ‘Diamond Platnumz’ na kudai staa huyo wa Wimbo wa Number One ni mzinzi ‘fuska’, Amani lina mkanda mzima.


Bila kumung’unya maneno, mapema wiki hii, Baby Madaha alimvaa Diamond ambaye ni Rais wa Wasafi Classic Baby (WCB) akimtuhumu kuwa na tabia za kifuska.
Baby Madaha alidai hata muziki anaoufanya Diamond kamwe hauwezi kulingana na mafanikio makubwa ya jina lake zaidi ya kubebwa na skendo tu.

CHOKOCHOKO ZILIVYOANZA
Kupitia mitandao ya kijamii, ilivuja posti ambayo ilidaiwa kutoka kwa Baby Madaha ikimpaka Diamond kuwa siyo mwanamuziki kama ilivyo kwa wasanii wengine wenye uwezo mkubwa, akitolea mfano Elias Barnaba wa THT.
Sehemu ya posti hiyo ilionesha kuwa, Diamond si msanii wa muziki bali ni mzinzi f’lani hivi anayefanya biashara ya muziki kupitia mapenzi.

“Siku wanawake maarufu nchini Tanzania watakapojitambua na kuacha kulewa penzi la Diamond, huo ndiyo utakuwa mwisho wa maisha yake kimuziki kwa sababu hatakuwa na jipya na hivyo soko lake litaporomoka,” ilisomeka posti hiyo.
UKWELI NI UPI?
Baada ya ishu hiyo kugeuka habari ya mjini na kuibuka kwa makundi mawili yanayokinzana, Amani lilimtafuta Baby Madaha ili kujua ukweli wa posti hiyo ndipo akatiririka aya za kuthibitisha kuwa picha haziivi, hamkubali Diamond na kudai hata kimuziki hamkubali kwani anaamini wapo wanamuziki wanaofanya vema katika gemu kuliko yeye.

“…tuseme ukweli, Diamond ni mfanyabiashara siyo mwanamuziki. Kuhusu hiyo posti iwe ni mimi nimeandika au si mimi lakini kimsingi hayo maneno yanamstahili kabisa. Mzinzi tu.
“Diamond anabebwa na media (vyombo vya habari). Kuna wanamuziki wengi wazuri sembuse yeye? Ana nini haswa?” alihoji Baby.

AMANI LAMGEUKIA DIAMOND
Baada ya kusikia maelezo ya Baby kwa kifupi, Amani lilimuweka ‘pending’ kwa muda na kumwendea hewani Diamond ili liweze kujua upande wake analizungumziaje bifu hilo ambalo lilikuwa likienea mitandaoni kama moto wa kifuu.
Tofauti na matarajio ya mapaparazi wetu kwamba huenda angejibu mashambulizi makali kwa Madaha, Diamond au ‘Sukari ya Warembo’ aling’aka huku akimponda mwanadada huyo na kumshangaa:

DIAMOND SASA
“Daaah! Huko ni kunishusha…mimi na huyo (Baby) wapi kwa wapi kamwe huwezi kunilinganisha na mtu ambaye yupo chini yangu sana, nikijibizana naye nitajishusha tu. Ingekuwa ni mtu mkubwa mwenye levo yangu hapo ningesema natakiwa kusema neno.
“Hana lolote huyo anatafuta ‘kiki’ tu kupitia mimi, nipo na dili zangu za maana nipoteze muda kwake? Atafute wa levo yake na wala si mimi.”

UZINZI VIPI?
Alipoulizwa kuhusu suala la uzinzi ambalo Baby Madaha aliumaanisha katika posti yake, Diamond aliendelea kukazia kuwa hana muda wa kupoteza kwa mtu kama Baby Madaha ambaye kimsingi ni kama ardhi na mbingu.
“Huyo anatafuta kiki tu, aachane na mimi…mbona hatufanani kabisa mimi na yeye wapi kwa wapi?” alikazia Diamond a.k.a Weka Mbali na Watoto Wazuri wa Kike.

BABY AREJEA HEWANI
Wakati mapaparazi wetu wakimalizana na Diamond, kilongalonga kimoja cha paparazi wetu kilikuwa kikionesha kinaita, ilivyokatika ya Diamond, Baby akapanda hewani kwa mara nyingine.

Safari hii alimchana laivu: “Nimeisoma upya posti yenyewe, kilichopo humu ni ukweli mtupu. Hakuna hata tone la uongo, wewe utamlinganisha Diamond na mtu kama Barnaba? Huyu ni mfanyabiashara tu, hajui kuimba kwa kutumia vyombo kama mimi.
“Diamond hawezi kupiga chombo hata kimoja cha muziki atajiitaje mwanamuziki? Anastahili kabisa ujumbe huu.”

UFUSKA
Mapaparazi wetu walilazimika kumtwanga swali Baby Madaha kuhusiana na ufuska ambao ulikuwa umetajwa katika maelezo ya awali, kama endapo Diamond ni mzinzi au yeye ndiyo mzinzi.
Katika maelezo yake, Baby Madaha aliwashangaza mapaparazi wetu kwa kutaja namna gani anaweza kumuita Diamond mzinzi. Sikia:

Amani: “Umesema Diamond si mwanamuziki, je, suala la uzinzi ni nani analo kati yako na yeye?”
Baby: “Mimi si mzinzi. Diamond ndiyo mzinzi tena sana tu.”
Amani: “Uzinzi wake upo wapi?”
Baby: “Kitendo cha kubadilisha wanawake, kufumaniwa na Wema Sepetu akiwa na Jokate Mwegelo ndiyo uzinzi wenyewe huo.”

Amani: “Kwani wewe hujawahi kuwa na wanaume tofauti? Hujawahi kufumaniwa?”
Baby: “Mimi sijawahi, yeye amewahi na hakuwahi kukanusha hivyo inadhihirisha kuwa ni kweli. Kwangu mimi kila aliyetajwa kutoka na mimi kama haikuwa kweli, nilikanusha mara moja yeye mbona hakanushi?”
Amani: “Kwani Diamond alifumaniwa na nani?”
Baby: “Acha hizo, kwani hukumbuki kipindi cha Wema? Mara alinaswa na Aunt mara na… yule ndiyo mzinzi sasa.”

KWANI WALITONGOZANA?
Kuhusu suala la kutongozwa, Baby alisema Diamond hajawahi. Cha kushangaza zaidi, alisema hata kama ikitokea siku staa huyo akamtongoza kamwe hawezi kumkubalia kwani hawaendani hata kidogo.
Alisema yeye ni mtu wa kutembea na vigogo na si vitoto kama Diamond.

“Hana hela, kamwe siwezi kumkubalia. Ni mtu ambaye ana vihela mbuzi sasa mtu kama yeye mimi wa nini? Ndiyo maana aliwahi kukimbiwa na mwanamke kwa kuwa hana hela.
“Tena yule mwanamke akaenda kwa kigogo mwenye hela, mimi na yeye ni mbalimbali kabisa. Hata muziki ninaofanya hauwezi, mimi ninaimba RnB yeye anafanya Pop, tuko tofauti kabisa,” alisema Baby pasipo kumtaja mwanamke aliyemkimbia Diamond.

TUJIKUMBUSHE PANDE ZOTE
Diamond aliwahi kuripotiwa kutoka kimapenzi na ‘totoz’ kibao wakiwemo yule wa mwanzo aliyemzingua aitwaye Sarah, Rehema Fabian, Jacqueline Wolper, Upendo Mushi ‘Pendo wa Maisha Plus’, Wema Sepetu, Natasha (Video Queen wa Wimbo wa Moyo Wangu), Najma (aliwahi kuwa mpenzi wa Mr. Blue), Jokate Mwegelo, yule demu wa Kenya na aliyekuwa mwigizaji aliyefulia ambaye ni mke wa mtu.

Kwa upande wake Baby Madaha anayekimbiza na ngoma yake ya Summer Holiday naye si haba kwani aliwahi kuripotiwa kuminya kimapenzi na yule mtoto wa mwanasiasa maarufu Bongo (jina lipo), Mwisho Mwampamba, Dokta Pakir, Juma Nature na Joe Kairuki aliye naye sasa ambaye ni mume wa mtu.

UKATILI! AMUUA MPENZI WAKE KWA KUMCHOMACHOMA NA KISU BAADA YA WAZAZI WA BINTI KUMKATAA ASIMUOE....

.

KIFO cha kikatili cha mwanafunzi aliyeuawa siku chache baada ya kuhitimu kidato cha nne katika Shule ya Sekondari Luguruni na mkazi wa Kimara Golani, Dar, Sharifa Rajab (18) bado ni simanzi nzito katika familia yake.
Sharifa aliuawa kikatili Novemba 22, mwaka huu, Kimara Golani jijini Dar na mtu anayedaiwa ni mpenzi wake ajulikanaye kwa jina la Abdul (22) ambaye ni dereva wa bodaboda.
SIMULIZI YENYE MAJONZI
Akizungumza kwa masikitiko makubwa, baba wa marehemu, Rajab Abdallah alisema siku ya tukio asubuhi, yeye na mke wake wakiwa kazini, Sharifa aliondoka nyumbani hapo  bila taarifa na kuwaacha wadogo zake tu.
“Tuliporudi jioni, mimi na mama yake tulianza kuhangaika kumtafuta bila mafanikio. Mwisho tuliamua kurudi kulala japokuwa usingizi ulikataa. Unajua tena mtoto ni mtoto. Huwezi kupata usingizi wakati mwanao hujui aliko.

“Tulipanga siku iliyofuata kwenda kutoa taarifa polisi, lakini ilipofika saa kumi na moja alfajiri, tuliletewa ujumbe kwamba kuna mwili wa mwanamke umekutwa kwenye chumba cha jirani.
“Ilikuwa vigumu kusema kwamba mwili huo ni wa mtoto wetu Sharifa, tuliamini kifo kipo, lakini watakufa wengine si mtoto wetu Sharifa.

“Hata hivyo, tulifunga safari kwenda kuuangalia mwili huo. Sikuamini hata kidogo nilipogundua kwamba ni mwanangu ndiye alilala kitandani, amekufa kwa kuchomwa kisu kooni na kwenye mbavu zote, kitanda chote kilijaa damu. Sharifa alikuwa si Sharifa tena bali marehemu Sharifa,” machozi yanamlengalenga.
Anaendelea: “Inaniuma sana! Mbaya zaidi nilijua  chumba hicho ni cha  kijana ambaye ni dereva wa bodaboda, anaitwa Abdul. Nikajiuliza ina maana alikuwa ni mpenzi wake? Sikupata jibu.”
TABIA YA MAREHEMU
Baba wa marehemu aliongeza kuwa, kwa kipindi chote cha uhai, Sharifa  hakuwahi kuonesha dalili kwamba alikuwa katika uhusiano wa kimapenzi, alikuwa ni msiri sana.

MTUHUMIWA WA MAUAJI AACHA UJUMBE
Habari zaidi zilidai kuwa, baada ya mtuhumiwa huyo kutekeleza mauaji ya binti huyo aliacha ujumbe wa maandishi akisema kuwa watu wasihangaike kumtafuta kwani na yeye anakwenda kujiua.
Hata hivyo, mtuhumiwa hakwenda kujiua, badala yake alifika Kituo Kikuu cha Mabasi ya Mikoani (UBT) kutafuta usafiri wa kurudi kwao Tanga lakini alipokosa aliamua kujisalimisha katika Kituo cha Polisi Ubungo na kukiri kuua.

Mmoja wa viongozi wa serikali ya mtaa (hakutaka kutaja jina lake) alisema mtuhumiwa huyo alipohojiwa polisi alisema hajui kilichotokea, akaomba apewe nafasi akamzike mpenzi wake huyo.

KAMANDA WA POLISI
Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi Kinondoni,  ACP Camilius Wambura alithibitisha kutokea kwa mauaji hayo ambapo alisema kwa mujibu wa mtuhumiwa alifanya kitendo hicho kutokana na wazazi wa msichana huyo kukataa yeye asimuoe na tayari alikuwa na mchumba mwingine.

Marehemu Sharifa alizikwa Novemba 24, mwaka huu katika Makaburi ya Golani Nzasa, Dar. Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi. Amina.

GPL

SINTAH NAYE AFUNGUKA BAADA YA IRENE UWOYA KUAMBULIA MAKAVU LIVE HAPO JANA....

.
Sintah amefunguka katika blog yake kuhusu mwanadada Irene Uwoya kubugi siku ya jana na kuweka Picha ya Vin Diesel akidhani ni Paul Walker. Soma hapo chini alichokisema

Van Diesel ambaye
Irene alifikiri ni Paul Walker

Let me a shame the devil, mara nyingi wanapokufa mastaa wa nje jamani ktk mitandao ya jamii tunakufa mbavu, sasa watu ndio kujifanya wanamjua sana watasononeka kiasi kwamba utafikiri ni ndugu wa damu,.
sasa afe star wa kwetu mmmmh hauoni hilo vumbi kama la nje jamani tujaribu kupenda na kuthamini vya kwetu vikiwa hai na vikitutoka sio kujishauwasti tujuwesti na wewesti unamjuasti paul walkerst kumbest nop
poor Irene amaejikuta akizodolewa, kwa kuchapia sasa sijui alitaka  aonekane anawajua  Hollywood celebrities  very well akajikuta anakosea baada ya kuweka pic ya Van Diesel na si ya Paul Walker aliefariki na kusisitiza bwana ametoa na bwana ametwaa..
 calm down, don't try so hard to fit in the cycle...... kama ni no ni NO tu...

I do the seeking n you do the judging

MADIWANI CCM,CHADEMA WAPIGANA NGUMI KAVUKAVU KISA KUHOJI MATUMIZI YA MILIONI 95/-......

 .
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mbeya,Diwani Athuman
Madiwani wawili wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) katika Halmashauri ya Jiji la Mbeya, wamejeruhiwa vibaya hadi kulazwa katika Hospitali ya Rufaa Mbeya kwa kile kinachodaiwa kupigwa na wenzao wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika eneo la ukumbi wa halmashauri wa Mkapa wakati kikao.
Diwani wa Kata ya Mwakibete ambaye pia ni Katibu wa Mwenezi Chadema wilaya ya Mbeya Mjini, Lucas Mwampiki, jana aliwaeleza wandishi wa habari kuwa tukio hilo lilutokea Ijumaa iliyopita katika ukumbi wa Mkapa ambao unamilikiwa na Halmashauri ya Jiji la Mbeya.

Mwampiki aliwataja madiwani waliojeruhiwa na kulazwa kuwa ni wa Kata ya Sinde, Fanuel Kyanula na wa Kata ya Ilemi, Furaha Mwandalima.

Mwampiki alisema kabla ya kutokea kwa vurugu hizo, madiwani wa vyama vya upinzani walikuwa wakihoji uhalali wa ziara ya baadhi ya maofisa wa Halmashauri ya Jiji wakiongozwa na Meya wa Jiji la Mbeya, Athanas Kapunga, kwenda China kwa kutumia fedha za halmashauri bila kufuata utaratibu.

Alisema katika ziara hiyo, Meya Kapunga aiongozana na maofisa watano ambao ni Mkurugenzi wa Jiji, Mchumi, Afisa Mipango na diwani mmoja wa CCM ambayo iliigharimu halmashauri hiyo zaidi ya Sh. milioni 95 ambazo hazikuwa kwenye bajeti wala kuidhinishwa na kikao chochote.

Alisema madiwani wa Chadema na NCCR-Mageuzi walifuata taratibu zote za kuhoji suala hilo, ikiwa ni pamoja na kuorodhesha majina yao na kusaini ili mkutano wa madiwani uitishwe na hoja hiyo ijadiliwe.

Kwa mujibu wa Mwampiki, kikao cha Madiwani kilichoketi Ijumaa waliamini kuwa ajenda hiyo itaingizwa, lakini wakashangaa kuona haimo kwenye orodha ya ajenda zilizopaswa kujadiliwa.

Alisema madiwani wa upinzani walipohoji juu ya kuondolewa kwa ajenda hiyo, Meya Kapungu ambaye alikuwa Mwenyekiti wa kikao hicho, alikuja juu na kuamuru mlango ufungwe ili madiwani wapigane.

“Tulishangaa kusikia Meya akisema kuwa kila siku madiwani wa Chadema tunawafanya wasiishi kwa raha mjini na kutamka kuwa inabidi milango ifungwe ili zipigwe,” alisema Mwampiki.

Alisema madiwani wa Chadema kuona hivyo waliamua kutoka haraka nje ya ukumbi wa mkutano, huku wakirushiwa chupa za maji na baadhi ya madiwani wa CCM.

Mwampiki alidai kuwa hata baada ya madiwani wa Chadema kuwa wametoka nje ya ukumbi wa mkutano, madiwani wa CCM waliwafuata na kuanza kuwashambulia kwa kipigo mpaka walipoachanishwa na polisi waliokuwepo eneo hilo.

Alisema katika vurugu hizo, madiwani wawili wa Chadema walijeruhiwa vibaya na kukimbizwa katika Hospitali ya Rufaa kwa matibabu na walilazwa.

Asema Diwani wa Ilemi, Mwandaliwa alijeruhiwa sehemu za shingo kiasi cha shingo yake kutogeuka kila upande huku Diwani wa Sinde, Fanuel akiwa amejeruhiwa kwenye shavu kutokana na ngumi walizokuwa wakipigwa.

Akizungumza baada ya kutoka hospitali, Mwandalima alisema alikuwa miongoni mwa madiwani wa mwisho kutoka ukumbini na kuwa alipofika nje ya ukumbi alijikuta akivamiwa na kundi la madiwani wa CCM ambao walianza kumshushia kipigo huku wengine wakimkaba na kumuumiza vibaya maeneo ya shingoni.

Meya wa Kapunga alikanusha kuhusika na ugomvi huo huku akisema kuwa hakuna diwani aliyepigana ndani ya ukumbi wa mkutano.

Alisema anachokumbuka ni kwamba madiwani wa upinzani walikuwa na hoja ya kutaka kujua juu ya ziara ya watumishi wa Halmashauri nchini China, lakini hawakufuata utaratibu na kanuni  walizojiwekea katika kuhoji masuala mbalimbali ya halmashauri.

Alisema baada ya kupitia orodha ya majina ya madiwani waliokuwa wakihoji suala hilo, walibaini kuwa kuna baadhi ya saini za madiwani zimeghushiwa, jambo ambalo alisema ni kinyume cha taratibu za halmashauri na sheria za nchi.

Alisema miongoni mwa saini zilizobainika kughushiwa ni za baaadhi ya madiwani ambao hawapo jijini Mbeya kwa muda mrefu.

Alisema baada ya hoja ya madiwani hao kukataliwa, ndipo walipoinuka kutoka ndani ya ukumbi wa mikutano huku wakiwatolea matusi ya nguoni madiwani wenzao wa CCM.

“Ninachokumbuka ni kwamba wakati madiwani wa Chadema wakitoka nje walikuwa wakitukana matusi ya nguoni inawezekana matusi hayo yaliwauma wenzao wa CCM ambao waliwafuata huko nje, hivyo kama walipigwa nje ya mkutano mimi sina taarifa,” alisema Kapunga.

Akizungumzia ziara ya watumishi wa halmashauri ya akiwamo yeye nchini China, Kapunga alisema ziara hiyo ilitokana na agizo la serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa  (Tamisemi).

Alisema kabla ya kufanya ziara hiyo alifuata taratibu zote ikiwa ni pamoja na kulijulisha Baraza la Mdiwani la Halmashauri ya Jiji la Mbeya, Ofisi ya Katibu Tawala ya Mkoa wa Mbeya, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa na Ofisi ya Waziri Mkuu, Tamisemi.

Naye Mkurugenzi wa Jiji la Mbeya, Mussa Zungiza, alipinga kiwango cha fedha cha Sh. milioni 95 kinachodaiwa na madiwani wa Chadema kuwa kilitumika kwenye ziara hiyo, badala yake alisema zilitumika Sh. milioni 54.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mbeya, Diwani Athuman, alipoulizwa kuhusu suala hilo, alisema yuko nje ya Mkoa wa Mbeya kikazi, hiyo hakuwa na taarifa zozote.

Pamoja na Kamanda Diwani kusema hana taarifa, lakini Mwandalima alisema walipewa fomu za polisi PF 3 kabla ya kupatiwa matibabu hospitali.

CHANZO: NIPASHE

"NIACHENI NA CHUCHU WANGU,KIFUPI NDIYE MKE WANGU...." RAY AFUNGUKA BAADA YA KUWA NA SKENDO YA KUTEMBEA NA CHUCHU MKE WA MTU

 .
Akizungumza wikiendi iliyopita katika Viwanja vya TCC Chang’ombe jijini Dar es Salaam ambapo kulikuwa na mechi kati ya wasanii wa Bongo Fleva na Bongo Muvi, Ray aliwashangaa waandishi kwa kumshambulia kutoka kimapenzi na Chuchu.
 
Mwandishi alianza kwa kumwuliza: “Ray magazeti yanaandika kuhusu wewe kutoka na Chuchu Hans ambaye ni mke wa mtu. Mainda amezungumza mengi. Kukaa kwako kimya bila kufafanua chochote siyo kitu kizuri. Tafadhali, hebu zungumza japo kidogo kuhusu madai ya Mainda.”
RAY: Sikia nikuambie, huyo Mainda utoto unamsumbua. Haniumizi kichwa kabisa. Kuhusu Chuchu... si mmeshaandika? Endeleeni kuandika lakini soon mtashuhudia kitu kikubwa sana.

RISASI: Ni kitu gani hicho?
RAY: Niacheni na Chuchu wangu.... kifupi ndiye mke wangu na itawashangaza wengi. Halafu mimi nawashangaa sana. Yaani mimi kutoka na Chuchu mnakuzaaaa... mbona alivyokuwa na ma-boyfriend zake wengine hamkuandika? Kwa sababu ni Ray basi mkaona ni habari. Mimi ninavyojua Chuchu siyo mke wa mtu.
Kwanza mimi sijamchukua kutoka mikononi mwa mumewe kama mnavyosema. Chuchu tayari alikuwa na maisha yake mapya. Nilimchukua kutoka kwa Libert (hajafafanua zaidi ni nani). Mbona alivyokuwa na huyo Libert  hamkuandika? Kifupi niacheni na maisha yangu.
RISASI: Vipi kuhusu Johari?
RAY: (Huku akikimbia kuingia uwanjani) Tena huyo mama yako (akimuonesha mwandishi Johari) anakuja.
Mwandishi wetu aliachana na Ray aliyekuwa akiingia uwanjani na kumfuata Johari lakini hakuwa tayari kusema chochote achilia mbali hata kumsikiliza mwandishi wetu!

TUJIKUMBUSHE
Hivi karibuni gazeti hili liliandika habari yenye kichwa MAINDA: NIMETOA MIMBA YA RAY. Ndani yake Mainda alifunguka mengi ikiwemo kuchanganywa kimapenzi na Ray, yeye na wenzake Johari na Chuchu Hans.
CREDIT:GPL

DIAMOND HAJUI KUIMBA NDIYO MAANA AMEKUWA MSANII WA MATUKIO HUKU NYOTA YAKE IKIEGEMEA KWENYE MAPENZI NA WASICHANA WENYE MAJINA MAKUBWA" BABY MADAHA

.

MSANII filamu na muziki wa kizazi kipya wa Tanzania Baby Joseph Madaha maarufu kwa jina la (Baby Madaha) amesema kwamba msanii mwenzake wa muziki nchini,Naseeb Abdul maarufu kwa jina la Diamond Platinumz si msanii bali ni mfanyabiashara. 

Madaha amesema kwamba Diamond si mwanamuziki na kamwe huwezi kumlinganisha na msanii kama Barnaba Boy, anayefanya muziki kama sanaa na kazi kulingana na kipaji chake na kwamba Diamond si msanii wa muziki bali ni msanii wa ngono anayefanya biashara ya muziki kupitia mapenzi.

Baby madaha ambaye hivi sasa yuko nchini Kenya kwa shuguli za muziki amesema kwamba, Diamond hajui kuimba na ndiyo maana amekuwa msanii wa matukio huku nyota yake ikiegemea kwenye mapenzi na wasichana wenye majina makubwa hususani wasanii.
Akizungumza na kandili yetu katika mahojiano maalum leo baby Madaha alisema kwamba, "Binafsi niliposikia kwamba Diamond anaumiza kichwa kunasa penzi la msanii Elizabeth Michael maarufu kwa jina la (Lulu) sikushangaa hata kidogo. kwa sababu nilitambua kwamba soko lake la muziki limeanza kushuka hivyo lazima atafute eneo lingine la kujiimarisha kibiashara, ili jina lake liendelee kuwika". 

"Siku wanawake maarufu nchini Tanzania watakapo jitambua na kuacha kulewa penzi la Diamond ndiyo itakayokuwa mwisho wa maisha yake kimuziki,kwa sababu hatakuwa na jipya na hivyo soko lake litaanza kuporomoka"alifafanua Baby Madaha

RAIS KIKWETE AMCHAGUA DR ASHA-ROSE MIGIRO KUWA MBUNGE....

THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

Telephone: 255-22-2114512, 2116898
E-mail:  ikulumawasiliano@yahoo.com
              press@ikulu.go.tz             

Fax: 255-22-2113425



PRESIDENT’S OFFICE,
      THE STATE HOUSE,
              P.O. BOX 9120,  
DAR ES SALAAM.
Tanzania.
 

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Dr. Asha-Rose Migiro kuwa Mbunge.
Taarifa iliyotolewa Ikulu, Dar Es Salaam leo, Jumanne, Desemba 3, 2013, na Kaimu Katibu Mkuu Kiongozi, Dr. Florens Turuka inasema kuwa uteuzi huo umeanza jana, Desemba 2, 2013.
Dr. Asha-Rose Migiro ni Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa, Idara ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa katika Chama cha Mapinduzi.

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.

3 Desemba, 2013

"NI KWA WAPUMBAVU WANAOANDIKA UJINGA WANIKWAZE,KAMA HUNIPENDI U BETTER F**K OFF!" IRENE AFUNGUKA BAADA YA MASHABIKI WAKE KUMSHAMBULIA

 .
Hapo jana mwanadada Irene uwoya aligeuka mada ya mtandao mmoja maarufu wa kijamii baada ya kuweka picha ya mwigizaji wa marekani Vin Diesel ikiwa na maneno ya “R.I.P – Bwana ametoa na bwana ametwaa” kwa jamaa huyo kuwa amefariki kitu ambacho sio kweli na ndipo mashabiki walipoanza kumshambulia mwanadada huyo kuwa awe anafanya research na sio kupost vitu ambavyo havielewi il mradi amepost.


Chanzo nini?

Hivi majuzi wapenzi wa filamu walipata na msiba wa mwigizaji wa maarufu wa filamu ya fast and furious Paul Walker aliyefariki kwa ajali ya gari huko nchini marekani. Mwigizaji huyu alikuwa karibu sana na mwigizaji Vin Diesel ambaye aIrene uwoya aliweka picha yake kuwa amekufa na ndipo mashabiki walipomvaa kuwa aliyekufa ni Paul hivyo atumie google kufanya uchunguzi na sio kuandika mambo amabyo hayajui kama tunavyomnukuu shabiki mmoja akimchana live Irene
Clarah: JAMAN IMENBIDI NIPOST HII KITU COZ NLISHTUKA KWANZA LOH !! @ireanuwoyaonepiceintown (Jina analotumia irene kwenye mtandao huo wa kijamii)  HUYU KAKA ANAITWA VAN DIESEL NI ACTOR MKUBWA TU .HAJAFA JAMAN MAANA UMENISHTUSHA KUMPOST NA KUMWISH BWANA AMETOA NA BWANA KATWAA .JAMAN KUNA GOOGLE IMERAHISISHA MAMBO YOTE UNGEGOOGLE JINA LA PAUL WALKER SIDHAN KAMA UNGEKOSA.JAMAN TUWE MAKINI NA HIZI TAARIFA MAANA WENGNE TUNAPRESSURE.ILIBIDI NIANGALIE NEWS YOUTUBE KAMA KWELI HUYU KAFA NA KAFAJE KUMBE MWENZETU PICHA GONGANA !!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!"""""""!!!!!!!!! @vandiesel MAY GOD GIVE U LONG YEARS TO LIVE MAANA KUNA MASNURA HUMU

Irene ajibu

Baada ya comment za mashabiki hao kuwa nyingi ndipo Irene alioamua kuitoa picha hiyo na baadaye kuwapa makavu wote waliomponda kwa kuandika ujumbe huu…
Irene uwoya: Hiii msg nikwawale wapumbavu wanao andika ujinga ili wanikwaze....maana kuna mijitu haijui nimeandika vile coz yule nimtu wake wakaribu na ninampenda ndomana nime post....ila ile mijitu isio na akili inavamia tuuu....kwanza kama unaona unipend na unikubali u better f#k off...sihitaji mijitu miswahili humu...nataka watu wenye upeo na adabu....nadhan mnajijua na mme nisoma....mi siogop mtuuu....nakama itakuuma kunywa sumu ufe

Mashabiki wagoma kumuelewa, wazidi kumpa makavu zaidi

ROGER: Kubali tu ulikosea mama yaishe.... maana mi naweza nikakuambia Irene R.I.P... kisa Kanumba Kafa... kuwa mtu wa Karibu haimaanishi ndo umwambie yeye arest in peace na kuweka picha yake kabisa

Levyl: Sasa kwann kaitoa c angeaacha kama yuko ryte

MrslucaS: Umebugi kubali tuu pyeee

Dorryjacob:  Swry hakuna anayekuchukia tatizo ulikosea na binadamu hukose..ww ulipost hyo pic ukijua ni paul kumbe ni vian so mbona rahic tu, ungesema umekose tatizo hutaki kushindwa kumbe kuna watu pia humu pamoja kwamba si masuper star bt nao ni vichwa hawakubali mbona ni simple like dat..na ndio maana umeitoa hyo pic maana na ww umejua umekose! Na pia anamafans zake wanaompenda so hawafurah ulivyomtabiria kifo..pole mummy kama umekwazika

PICHA: AJALI MBAYA YA BASI LA URAFIKI...!!

.0 027b0
1 96a73

2 3f6b3
Wakazi wa kijiji cha Ndolela Tarafa ya Isimani wilaya Iringa vijijini wakiangalia ajali ya Basi la abiria la Urafiki  T 594 ABM lililoanguka kijijini hapo jana likitokea Iringa kuelekea Dodoma. PICHA NA SAID NG'AMILO.

 

Copyright © 2010 GUMZO LA JIJI.

Like Us On Facebook
Follow Us on Twitter