UTENGENEZAJI WA FAST AND FURIOUS 7 KUENDELEA BAADA YA KUSIMAMA KWA MUDA KUTOKANA NA KIFO CHA MMOJA WA MASTAA WAKE,PAUL WALKER....

Paul walker enzi za uhai wake
Utengenezaji wa filamu mpya ya Fast and Furious utaendelea licha ya kifo cha mmoja wa mastaa wake, Paul Walker. Utengenezaji wa filamu hiyo yenye bajeti kubwa ulikuwa umesimama weekend wakati wa sikukuu ya Thanksgiving ambapo Walker alipata ajali na kufa siku ya Jumamosi. Walker alikuwa arejee kuendelea na utengenezaji wa filamu hiyo jijini Atlanta nakuungana na mastaa wenzie Vin Deisel na Dwayne Johnson aka The Rock. James Wan, ambaye ni muongozaji wa filamu hiyo na wakurugenzi kutoka Universal Studios walifanya mkutano jana asubuhi kujadili jinsi ya kuendelea na Fast and Furious 7 katika njia ambayo itakuwa na heshima kwa kifo cha Walker. Kwa mujibu wa The Hollywood Reporter, kushoot kunaweza kuanza Jumanne hii. Walker alikuwa akiigiza kama Brian O'Conner, mhalifu aliyebadilika na kuwa polisi kwenye Fast and Furious 7, uhusika alioucheza katika filamu sita zilizopita za Fast and Furious. Shooting ya filamu hiyo itamalizka Januariy huko Abu Dhabi.
Fast and Furious 7 ilipangwa kutoka July 11, 2014.

Tupe maoni yako hapo chini..!

Share this article :

'LIKE' UKURASA WETU WA FACEBOOK HAPO CHINI...!

0 comments:

Post a Comment

TOA MAONI YAKO HAPA....

 

Copyright © 2010 GUMZO LA JIJI.

Like Us On Facebook
Follow Us on Twitter