Miss TANZANIA Salha Israel anusurika kuibiwa GARI usiku!

WATU wanaosadikiwa kuwa ni majambazi juzikati walivamia nyumbani kwa Miss Tanzania 2011, Salha Israel maeneo ya Sinza-Mori jijini Dar na kufanya jaribio la wizi.Akizungumza na Ijumaa, Salha alisema tukio hilo lilijiri hivi karibuni mishale ya saa 8:00 usiku ambapo watu hao wasiofahamika waliruka ukuta na kutaka kufanya uhalifu lakini walishitukiwa kabla ya kutekeleza mpango huo.

“Sijui niseme ni wezi au majambazi ila ilikuwa saa 8 usiku, watu hao waliruka ukuta wakaingia ndani. Hutujui kama walitaka kuondoka na gari au kuiba vitu vilivyokuwemo ndani yake lakini walivunja kioo cha mbele.
“Kwa bahati tulisikia vurugu zao na kabla ya kuiba chochote, tuliwakurupusha na ndipo walipokimbia,”
alisema Salha.

Tupe maoni yako hapo chini..!

Share this article :

'LIKE' UKURASA WETU WA FACEBOOK HAPO CHINI...!

0 comments:

Post a Comment

TOA MAONI YAKO HAPA....

 

Copyright © 2010 GUMZO LA JIJI.

Like Us On Facebook
Follow Us on Twitter